Breadcrumbs

PF-related

Taarifa ya Umma inayohusu Kukamatwa kwa Wanaharakati wa Haki za Binadamu

Mtandao wa Watetezi wa  Haki za Binadamu Tanzania (THRD-Coalition) unaoratibiwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Pamoja na mtandao wa asasi za kiraia wa Policy Forum wanatoa wito kwa Serikali kuwaachia mara moja Watetezi wa  haki za binadamu 16 ambao waliwekwa chini ya ulinzi mnano tarehe 9/2/2012 katika eneo la Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.  Tukio hilo  limekuja siku moja baada ya wanaharakati kuungana na  kuishinikiza serikali irejee mezani kufanya mazungumzo na madaktari  ambao kwa takribani mwezi mmoja sasa wameingia kwenye mgomo na kus

Utambulisho wa Filamu ya Kijiji cha Tambua Haki

Policy Forum kwa kushirikiana na Kanumba the Great Films wanayo furaha kuitambulisha kwenu filamu ya Kijiji cha Tambua Haki, filamu ambayo ina lenga kuelimisha jamii juu ya utawala bora na uwajibikaji katika ngazi ya serikali za mitaa hadi kitaifa.Utambulisho huu ulifanywa tarehe 8 Februari 2012 katika hoteli ya Regenct Park.

Kidokezi cha Filamu ya Kijiji cha Tambua Haki - Filamu ya Utawala bora na Uwajibikaji katika Jamii

Policy Forum kwa kushirikiana na Kanumba the Great Films wanayo furaha kuitambulisha filamu ya Kijiji cha Tambua Haki, Filamu ambayo inakusudia kuielimisha jamii mambo ya utawala bora na uwajibikaji katika jamii.

Tafadhali angalia kidokezi cha filamu hiyo.

Majadiliano juu ya nafasi ya Mazingira na Maliasili katika katiba mpya ya Tanzania

Tanzania inaelekea kipindi cha marekebisho ya kihistoria ya katiba yake, mchakato umeshika kasi kubwa baada ya uchaguzi mkuu wa 2010. mchakato wa marekebisho haya yanayoendelea kwa kiasi kikubwa umeweka mbele masuala ya kupunguza nguvu za rais, haja ya kubadili Tume ya Taifa ya Uchaguzi, suala la haja kwa wagombea binafsi, na uchaguzi huru na wa haki. Kipaombele kidogo sana, hata hivyo, kimewekwa kwa upande wa kuingiza masuala ya mazingira na maliasili katika katiba. Kama wote tunavyojua, haya ni ya msingi kwa ustawi wa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

Semina ya Ukwepaji Haramu wa Mitaji Iliyofanyika Mwanza

 

Alex Ruchyahinduru, Meneja wa Mawasiliano na Uchechemuzi wa Policy Forum akiwasilisha mada

Mnamo tarehe 29 Novemba 2011 kulikuwa na semina ambayo iliyoandaliwa na Forum Syd, Mwanza Policy Initiative na Policy Forum ya  ukwepaji haramu wa mitaji katika nchi maskini iliyofanyika Victoria Palace Hotel, Mwanza.

TAMKO KUHUSU UWAZI KATIKA BAJETI, UWAJIBIKAJI NA USHIRIKISHWAJI

Sisi ni nani
Sisi ni raia na asasi za kiraia kutoka kote duniani, ambao tumeunganishwa na imani kwamba uwazi na ushirikishwaji katika bajeti  za umma ni muhimu sana katika kujenga dunia ambayo binadamu wote wanafurahia haki zao za binadamu- kiraia, kisiasa, kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kimazingira.

Tangazo la Policy Forum la Uwazi na Uziduaji katika Sekta ya Madini

Policy Forum imetoa tangazo juu ya Sekta ya nishati na madini Tanzania ambalo kwa sasa linarushwa hewani katika vituo viwili vya Televisheni ambavyo ni ITV na Star TV. Lengo la tangazo ni kuwafanya raia wa kawaida wa Tanzania kuuliza viongozi wao juu ya rasilimali ya madini yao ambayo inapaswa kutumiwa kwa manufaa ya watanzania na si vinginevyo. Ona tangazo chini

Video ya mashirika ya kiraia yakishirikiana na Bunge katika kuboresha sheria ya madini Tanzania

Mwaka 2010, viongozi wa mashirika yasiyo ya kiserikali walishirikiana na Bunge katika kuboresha sheria ya madini ya Tanzania. Hii filamu fupi ya Revenue Watch International inaonyesha<

Tamko la Ngurdoto la Kamati ya Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia Oktoba 20, 2011

Sisi, Kamati ya Viongozi wa Dini kwa Masuala ya Kijamii, Uchumi, Haki na Uhifadhi wa Mazingira na Maumbile na wanachama wa Policy Forum, tuliokutana katika Mkutano Mbadala wa masuala ya Madini mjini Arusha tarehe 20 Oktoba 2011, tumejadili kwa kina madhara yatokanayo na shughuli za uchimbaji wa madini katika jamii zionazoishi karibu na migodi ya madini na kwa mazingira, na tunaiomba serikali na Bunge kuhakikisha kuwa zinatekeleza kwa dhati majukumu yao kwa kuhakikisha kuwa haki za wananchi ambao hawajanufaika na s

Policy Forum Kushiriki katika semina ya asubuhi ya ukwepaji haramu wa mitaji katika nchi maskini iliyofanyika sweden

 

 

Moses Kulaba, Mwakilishi wa kikundi kazi cha bajeti akiwa anatoa mada Stockholm tarehe 23 Septemba