Latest news

Mazungumzo ya Asasi za Kiraia Juu ya Ukwepaji Haramu wa Fedha Afrika

Wiki hii Policy Forum ilifanya mjadala maalum wa nusu siku kuhusiana na ukwepaji haramu wa fedha kutoka Afrika na wataalamu wawili wa kimataifa wa mada hii ambao ni Baker Raymond, Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Financial Intergrity,taasisi inayoongoza ya kimataifa ya uchunguzi wa fedha haramu  uliounganishwa na Alvin Mosioma, Mratibu wa Tax Justice Network Afrika, taasisi ambayo ina lengo la kukuza haki za kijamii, kidemokrasia na maendeleo ya mifumo ya kodi ya Afrika.

Bodi Mpya ya Wakurugenzi ya Policy Forum ya Mwaka 2012

Kuhama kwa Ofisi za Policy Forum

Hii ni taarifa kwa wanachama wa Policy Forum na umma kwa ujumla kuwa kuanzia Machi 12, 2012, ofisi ya Policy Forum itahama kutoka Plot 270 Kiko Avenue, Hivyo anwani yetu mpya itakuwa:

 Plot 14, Nyumba No. 752
 Sembeti Street (Off Old Bagamoyo Road)
 Mikocheni B
 Dar es Salaam

 Anwani yetu ya posta, barua pepe, tovuti na namba ya Mkono zinabakia vile vile

 Namba yetu mpya ya simu ni +255 22 2780200

 Wapi tunaweza kupatikana?

Taarifa ya Umma inayohusu Kukamatwa kwa Wanaharakati wa Haki za Binadamu

Mtandao wa Watetezi wa  Haki za Binadamu Tanzania (THRD-Coalition) unaoratibiwa na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Pamoja na mtandao wa asasi za kiraia wa Policy Forum wanatoa wito kwa Serikali kuwaachia mara moja Watetezi wa  haki za binadamu 16 ambao waliwekwa chini ya ulinzi mnano tarehe 9/2/2012 katika eneo la Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam.  Tukio hilo  limekuja siku moja baada ya wanaharakati kuungana na  kuishinikiza serikali irejee mezani kufanya mazungumzo na madaktari  ambao kwa takribani mwezi mmoja sasa wameingia kwenye mgomo na kus

Utambulisho wa Filamu ya Kijiji cha Tambua Haki

Policy Forum kwa kushirikiana na Kanumba the Great Films wanayo furaha kuitambulisha kwenu filamu ya Kijiji cha Tambua Haki, filamu ambayo ina lenga kuelimisha jamii juu ya utawala bora na uwajibikaji katika ngazi ya serikali za mitaa hadi kitaifa.Utambulisho huu ulifanywa tarehe 8 Februari 2012 katika hoteli ya Regenct Park.

Kidokezi cha Filamu ya Kijiji cha Tambua Haki - Filamu ya Utawala bora na Uwajibikaji katika Jamii

Policy Forum kwa kushirikiana na Kanumba the Great Films wanayo furaha kuitambulisha filamu ya Kijiji cha Tambua Haki, Filamu ambayo inakusudia kuielimisha jamii mambo ya utawala bora na uwajibikaji katika jamii.

Tafadhali angalia kidokezi cha filamu hiyo.

Majadiliano juu ya nafasi ya Mazingira na Maliasili katika katiba mpya ya Tanzania

Tanzania inaelekea kipindi cha marekebisho ya kihistoria ya katiba yake, mchakato umeshika kasi kubwa baada ya uchaguzi mkuu wa 2010. mchakato wa marekebisho haya yanayoendelea kwa kiasi kikubwa umeweka mbele masuala ya kupunguza nguvu za rais, haja ya kubadili Tume ya Taifa ya Uchaguzi, suala la haja kwa wagombea binafsi, na uchaguzi huru na wa haki. Kipaombele kidogo sana, hata hivyo, kimewekwa kwa upande wa kuingiza masuala ya mazingira na maliasili katika katiba. Kama wote tunavyojua, haya ni ya msingi kwa ustawi wa Watanzania na jumuiya ya kimataifa kwa ujumla.

Kufungwa kwa ofisi ya PF Sekretariati

Tunapenda kuwataarifu kuwa ofisi ya Sekretarieti ya Policy Forum itafungwa  kwa likizo ya Krismasi na Mwaka Mpya kuanzia Desemba 20, 2011 Jumanne hadi Ijumaa  Januari 6, 2012.

Ofisi itafunguliwa na kuanza tena shughuli zake za mara kwa mara tarehe Jumatatu Januari 9, 2012.

Semina ya Ukwepaji Haramu wa Mitaji Iliyofanyika Mwanza

 

Alex Ruchyahinduru, Meneja wa Mawasiliano na Uchechemuzi wa Policy Forum akiwasilisha mada

Mnamo tarehe 29 Novemba 2011 kulikuwa na semina ambayo iliyoandaliwa na Forum Syd, Mwanza Policy Initiative na Policy Forum ya  ukwepaji haramu wa mitaji katika nchi maskini iliyofanyika Victoria Palace Hotel, Mwanza.

TAMKO KUHUSU UWAZI KATIKA BAJETI, UWAJIBIKAJI NA USHIRIKISHWAJI

Sisi ni nani
Sisi ni raia na asasi za kiraia kutoka kote duniani, ambao tumeunganishwa na imani kwamba uwazi na ushirikishwaji katika bajeti  za umma ni muhimu sana katika kujenga dunia ambayo binadamu wote wanafurahia haki zao za binadamu- kiraia, kisiasa, kijamii, kiuchumi, kiutamaduni na kimazingira.

RSS feed
[?]
RSS Feed
How to use RSS feed - click here for more info and help