Dira: Policy Forum ni asasi huru yenye dhamira ya kuhusisha wananchi, asasi zisizo za kiserikali, na sekta zote zingine za jamii katika michakato ya uundwaji wa sera. Dhamira hii pia inahusisha kuwezesha hatua zote za michakato ya uundwaji wa sera zinaelimisha wananchi, zinakuza uwezo wao wa kujihusisha na zinaendeshwa kwa njia inayotoa nafasi ya uwajibikaji.

Ripoti ya Bomani - Taarifa fupi ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini


Policy Forum tunayo furaha kuchapisha kitabu hiki ambacho kinatokana na ‘Taarifa ya Kamati ya Rais ya Kuishauri Serikali Kuhusu Usimamizi wa Sekta ya Madini’ Juzuu Namba 2.

Shukrani kwa Reginald Martin wa LHRC kwa ushirikiano wake wa hali na mali ikiwa ni pamoja na kutumia muda wake kuhakikisha anaihariri Taarifa hii fupi. Bila kumsahau mchora katuni wetu Nathan Mpangala.

Msimamo wa Wanachama wa Policy Forum kuhusu Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo

1.0 UTANGULIZI    Wanachama wa Policy Forum, tukiwa ni sehemu ya jumuiya za kiraia na sehemu ya wapiga kura wa wabunge wetu tumechukua jukumu katika jukwaa hili leo kutoa tahadhari kwa wabunge wetu kuhusu athari za kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo ya jimbo. Hii ni sehemu muhimu ya wajibu wetu kama raia waaminifu, wenye nia njema ya kuchangia mawazo bora yatakayotuletea maendeleo endelevu nchini kwetu.

Warsha ya Uwajibikaji Jamii katika Mkoa wa Mwanza

mwanza_mpi 045.JPG
Bw. Angelo wa PF akitoa mada

Ikishirikiana na Mwanza Policy Initiative (MPI), wiki hii Policy Forum inaendesha warsha kuhusu Uwajibikaji Jamii (Social Accountability Monitoring – au kwa kifupi, SAM) kwa ajili ya asasi za kiraia za Mwanza.

Warsha hii imeanza tarehe 28 Julai hadi Agosti Mosi na ni moja kati ya malengo ya Policy Forum ya kusaidia kuboresha uwezo wa asasi za kiraia kuelewa, kufuatilia, kushiriki kwa ufanisi, na kushawishi michakato ya sera za kitaifa na zile za ngazi ya serikali za mitaa.

RSS feed
[?]
RSS Feed
How to use RSS feed - click here for more info and help